Sunday 18 October 2015

SOMO LA NIDHAMU YA UPIGAJI KURA KWA VIJANA.

Takribani siku saba (7) zimesalia kuipata hatima ya taifa letu lenye amani TANZANIA. Katika duru za siasa kumeonekana kuwemo upinzani mkubwa baina ya chama tawala CCM na CHAMA CHA DEMOKRASIA NA MAENDELEO kupitia mgombea wake EDWARD NGOYAI LOWASSA chini ya ,mwavuli wa umoja wa katiba ya wananchi UKAWA ukijumuisha muungano wa chama cha NSSR, NLD, CUF na CHADEMA. Wingi wa idadi kubwa ya umati wa watu mamia kwa maelfu katika kampeni za CHAMA CHA CHADEMA. ni moja ya sababu ya kuiletea matumaini makubwa na kukipa uhai chama.Kwa kuridhika na hili MH.EDWARD LOWASSA anaweza kujipa asilimia 90% za ushindi hata kabla ya siku ya upigaji kura.. 
ZINGATIA: 
Tukumbuke idadi kubwa ya vijana wameonesha hamasa kubwa katika zoezi zima la uandikishaji wa daftari la kudumu la wapiga kura.Wakiwa na matamanio makubwa ya siku ya upigaji kura kumchagua RAIS, MBUNGE NA DIWANI. wengi wetu wakiwa na fikra za MABADILIKO. JE? MABADILIKO haya yatawezekana pasipo kuhakikisha unapiga kura katika hali ya nidhamu na kufuata taratibu zote za upigaji wa kura! Ushindi wa mabadiliko umeshaonesha mwangaza, hivyo basi pasipo kufifisha mwangaza na nuru ya ukombozi ilioletwa na MH EDWARD LOWASSA, hatuna budi kuwapa elimu vijana juu ya nidhamu, taratibu na sheria za upigaji kura kwani wengi wao ni mara yao ya kwaanza kuingia kwenye chumba cha upigaj kura. Fomu za mifano zitumike kuwafikia na kufundishia vijana juu ya namna sahihi ya kukitumia kikatio chako! Kura ni HAKI YAKO YA MSINGI. KURA VYAKO MOJA INAWEZA KUYABADILISHA MATOKEO YA UCHAGUZI.ITUMIE VIZURI NAFASI HIYO KUWAWAKILISHA WATOTO NA WENGINE WASIONA SIFA ZA KUPIGA KURA. Kuzingatiwa kwa hili CHADEMA watakua wamejihakikishia ushindi mnono pasi na shaka.
 (MUHIMU)
Baada ya kuweka tiki kwa  mgombea wako uliempigia kura hakikisha hauchafui karatasi ya kupigia kura kwa kuichora au kuandika kitu chochote kwani kwa kufanya hivo utakuwa umeharibu kura yako na utakuwa umejikosesha haki yako ya msingi
   
MAMBO YA KUYAEPUKA SIKU YA KUPIGA KURA
  
1-Baada ya kumaliza kupiga kura toka nje bila kubuguzi watu wengine wanaohitaj kupiga kura kama ulivofanya wewe

2-Hakikisha hauvai sare ya chama chochote huenda ikawa ni Chadema, Cuf, Ccm, Act maana kwa kufanya hivo kutaweza kusababisha usipige kura yako na ukawa umejikosesha haki yako ya msingi.

3-Epuka kuweka vikundi katika maeneo ya kupiga kura yenye lengo la kuhamasisha wananchi wenzio wampigie kura mgombea gani.

4-Hakikisha baada ya kupiga kura unakaa mita 200 kutoka eneo ulilopigia kura ili kusubiria  matokeo ya uchaguzi uliofanya.
AKHSANTENI.

No comments:

Post a Comment