Wednesday 30 September 2015

MBINU BORA ZA KUKUPA MATOKEO CHANYA

         
Kuingia uraiani baada ya kumaliza masomo ya elimu ya juu Ni suala lenye uzito wake kwa idadi kubwa ya wanafunzi vyuoni. Kufanyia kazi masomo uliyosomea darasani kwa nadharia. Pasipo muda wa kukusubiri, shinikizo la bosi na changamoto nyingi zilizopo maofisini. Pia ni muda huu tunapokosa uhuru wa kujipangia ratiba zetu binafsi.
Hizi ni baadhi ya mbinu bora za kukupa matokeo chanya katika maisha yako.
KUA NA RATIBA MAALUMU

Siri ya kufanya maisha yako yasiwe ya upweke na msongo wa mawazo juu ya ntapata wapi kazi, au ntafanya nini ili niweze kupata kipato baada ya kumaliza masomo yako ni kuandaa ratiba maalumu itakayojumuisha shughuli zako zote za kila siku kama ilivyokua kipindi upo chuoni. Kwa mfano kama ulikua unahudhuria mazoezi ya jioni kila siku baada ya masomo yako basi ni vivyo ivyo hata baada ya kumaliza masomo hakikisha unapotoka kwenye harakati zako za kila siku unaenda mazoezini kama siku zote.
USIWE NA SHAKA HATA KAMA HUJAPATA KAZI UNAYOITAMANI KATIKA MAISHA YAKO (DREAM JOB)
Hata kama si kazi yenye kukidhi mahitaji yako ya kila siku, usikatae kufanya kazi! Fanya kwa muda wakati uinaendelea na michakato mengine ya kutimiza ndoto zako. Kupata kazi moja kunafungua mianya ya kupata kazi nyingine. NUKUU YA USEMI WA WAHENGA “MTEMBEA BURE SIO SAWA NA MKAA BURE” kwa hili suala ata wewe huna budi kuwaunga mkono wahenga.
FAIDIKA NA RASILIMALI ZILIZOKUZUNGUKA
Licha ya maisha yetu ya kawaida ya kuzunguka sehemu mbalimbali. Hakikisha unazijua rasilimali zote unazopaswa kua nazo kwa kipindi icho kama mfanyakanzi katika kampuni husika. Usiogope kuuliza! (Kwani kuuliza si ujinga) Ukiwa kama mfanyakazi mpya unapaswa kuwa karibu na boss pamoja na wafanyakazi wenzako ili kuweza kupata taarifa zaidi juu ya masuala muhimu kufanikisha utendaji wako wa kazi.
Kwa mfano: upatikanaji wa chanzo cha mtandao (internet) na bima mbalimbali.

ONGEZA UMAKINI KATIKA MATUMIZI YA FEDHA.
Ulikua unaishi kwa tsh 10,000 kwa siku, hakikisha hauvuki kiwango kuzidi kipato chako cha siku cha kawaida. Na kama inawezekana nakushauri udumu katika kiwango ichoicho kwa muda flani mpaka pale vyanzo vya kipato vinapoongezeka. Lipa madeni,  endelea kuhifadhi fedha. Na kama unatumia kuzidi kipato chako, una hatari ya kutumbukia kwenye utumwa wa ajira kwa kipindi kirefu.
"Mtanzania wa kawaida anayeweza kumudu kupata tsh 5000 kwa siku. Akifanya matumizi ya tsh 4000 na kuweka akiba tsh 1000 kila siku.
Ni makadilio ya kuvuna tsh 365,000 kila mwisho wa mwaka.
1,825,000 ndani ya miaka mitano".
Je? Vp wewe msomi wa chuo kikuu uliyeibeba shahada ya kwanza ya sheria, ualimu, afisa masoko, afisa ugazi, afisa rasilimali watu au udaktari. Mwenye makadirio ya kuweza kumudu kupata tsh 10,000 kwa siku.
Hifadhi japo tsh 5000 tu kwa siku ili baadae ikuzalishie 1,825,000 ndani ya mwaka mmoja.
Makadirio ya kuvuna tsh 9,125,000 baada ya miaka mitano.
Hesabu hizi ni nje ya mshahara, vijibiashara vidogo vidogo na vyanzo vingine vinavyokuingizia kipato.
THAMINI NA IPENDE KAZI YAKO
Msingi imara wa kudumu katika utendaji, ni kuipa thamani kazi uliyoipata. Tambua ,manufaa yake ata kama ni kidogo kulingana na gharama za maisha zinazopanda kila kukicha. Jenga mawazo chanya, fanya kazi kwa muda husika, tengeneza mazingira rafiki ya kazi na hakikisha unajenga mahusiano mazuri na wafanyakazi wenzako. Ukizingatia haya nakuhakikishia mwanzo mzuri wa safari yako kuelekea kwenye kilele cha mafanikio.

JENGA MWILI NA AFYA YAKO
Suala la msingi zaidi ni afya tukizingatia afya ni uhai. Hakikisha unapata milo mitatu kila siku, kula vyakula vyenye virutubisho vya kujenga mwili na kuupa kinga dhidi ya magonjwa. Sambamba na matunda pia maji ya kutosha wakati wote. Mazoezi ni tatizo kubwa linalowakabili asilimia kubwa ya watanzania. Tukiwa na Imani ya kua mazooezi ni kwa ajili ya wana michezo tu! Mazoezi yatakufanya ujisikie mwepesi na mwenye afya tele usiye sumbuliwa na magonjwa madogomadogo.


JIFUNZE MAMBO MAPYA UNAPOPATA FURSA ZA KUSAFIRI SEHEMU MBALIMBALI.
Unaposafiri katika maeneo mapya hakikisha unaitumia vizuri fursa iyo kujifunza. Tembelea nyumba za makumbusho, mbuga kama zipo, soko, kanisa na misikiti. Jifunze tamaduni na desturi zao, namna jamii iyo inavyoendesha maisha yake ya kila siku. Na pia ijue mitaa yote iliyokaribu na unayoweza kumudu kuitembelea.

Jitambue!

Sual la mwisho la msingi ni kutambua ya kwamba muda nliokua naupoteza chuo, kwa hivi sasa una thamani ya hali juu kuikamilisha safari hii. Chuoni tulipata muda mwingi wa kuzurula na marafiki, kupika, kufua nk. Wengi wetu tulikua hatujui kama muda wa kufua au kupika unaweza ukawa na thamani mfano wa fedha tunayoitafuta. Nukuu kutoka kwa mwandishi.
MFANO:
DAKIKA MOJA INAWEZA KUWA NA THAMANI YA TSH 100 TU!
DAKIKA 60 ( SAA MOJA) IKIWA NI SAWA NA THAMANI YA TSH 6,000
DAKIKA 1440 ( MASAA 24)siku moja THAMANI YA TSH 144,000
Kwa makadirio haya wengi wetu tutatahamaki na kushika midomo baada ya kugundua tumeshapoteza mabilioni ya fedha tangu kujitambua kwetu. MUDA NI PESA! OKOA MUDA! TUNZA MUDA!








No comments:

Post a Comment